Tuesday 1 April 2014

VURUGU ZILIZOTOKEA MECHI YA KAGERA SUGAR NA RUVU SHOOTING, KRFA WAMEJIPANGAJE KWENYE MECHI YA KAGERA SUGAR NA SIMBA JUMAMOSI 5-4-2014 KAITABA?



Kijana wa  Kimasai alisababisha vurugu akiwa amezibitiwa na Polisi akiwa chini ya ulinzi

Wakati zikiwa zimesalia siku chache kufanyika mtanange mkali wa Kagera Sugar na Simba ligi kuu  vadacom  katika uwanja wa Kaitaba siku ya Jumamosi  5-4-2014 chama cha mpira  Mkoa wa Kagera kimejipangaje kuhakikisha kinathibiti vurugu zinazoweza kutokea na kusababisha kuhatarisha usalama wa mashabiki,Katika mechi ya Kagera Sugar na Ruvu Shooting iliyochezwa jumapili 30-3-2014 tumeshuhudia  vurugu zilizozukiwa na  Kijana mmoja wa kimasai aliemvamia shabiki mmoja alietambulika kwa jina la Moses Nyama  ambae ni msanii katika bend ya muziki ya Kakau kumpiga  akishilikiana na wenzake kwa fimbo huku wakiwa na siraha za visu viunoni na kumjerui kabla ya mashabiki kuingilia kati kumnusuru na badae Polisi kufika wakiwa wakitazama mpira badala ya usalama wa raia. Ili kuzibiti hali hii ya mashabiki kuingia uwanjani na fimbo, visu, mikuki nk KRFA na Jeshi la Polisi mmejipanga vipi katika mtanange wa Kagera Sugar na Simba Jumamosi 5-4-2014 ?

Huyu ni Mmasai ambae ni miongoni mwa waliojerui akiwa na sime kiunoni akizibitiwa na  Askari waliovaa kilaia






Mashabiki wanahitaji Amani wakati wote uwanjani


Shabiki nguli wa Simba MSHAMU




Mmasai akiwa kapandisha mzuka anataka kupiga mtu na wengine wakiwa wamedhibitiwa na Mashabiki







Wote hawa wamasai walivamia mtu mmoja kwa fimbo zao ,na kumjerui


Mwenye kaunda suti ni Katibu wa KRFA Salumu Chama alilazimika kuingilia kati sakata hili




Baada ya dakika kadha Polisi waliokuwa wakiangalia mpira walikuja baada ya mashabiki kupiga kelele . Na hapa ndio swala la kujiuliza na kufanyiwa kazi, je Polisi anapoingia uwanjani ni kwa ajili ya kuangalia mpira au usalama wa mashabiki? swali kwa wahusika.


Je kuingia na fimbo na visu uwanjani  ni sahihi?



Kulia ni Moses Nyama alipata kipigo kutoka kwa Wamasai Japo nae si haba MWANZONI alikabiliana nao.

No comments:

Post a Comment