Tuesday 31 December 2013

RAIS KIKWETE AKABIDHIWA RASIMU YA KATIBA (TOLEO LA PILI)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akipokea Rasimu ya pili ya katiba mpya kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba mpya, Joseph Warioba, wakati wa hafla ya kukabidhiwa rasimu hiyo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, leo. Akizungumza katika hafla hiyo Rais, aliitaka Tume hiyo kuiweka Rasimu hiyo kwenye mitandao ili wananchi waweze kuisoma na kuielewa na kuweza kutoa maoni yao kwa urahisi kupitia mitandao.
 Naye Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Warioba, alisema kuwa kulingana na idadi ya kura zilizopatikana kutoka kwa wananchi kuhusu uundwaji wa Serikali tatu, alisema kuwa idadi kubwa zaidi ni ya watu walihitaji Serikali tatu kuliko walioipinga, hivyo Serikali tatu haipingiki ambapo kwa sasa itabaki ni kazi ya maamuzi ya Bunge la Katiba linalotarajia kuungwa mapema mwezi Januari mwakani.
 Rais jakaya Kikwete, akimkabidhi raismu hiyo Makamu wake baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa Tume ta katiba mpya.
 Rais Jakaya Kikwete, akimkabidhi Risimu hiyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda na baadhi ya viongozi.
 Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa, waliohudhuria hafla hiyo.
 Baadhi ya waasisi waliokabidhiwa Rasimu hiyo na Rais kikwete, baada ya kukabidhiwa.
 Tundu Lissu, na wenzake wakiangua kicheko baada ya kutaniwa na Rais wakati akisoma hotuba yake kwenye hafla hiyo.
 Zitto Kabwe, akiisoma Rasimu hiyo kwa makini.......
 Jaji Warioba, akimkabidhi Rasimu hiyo, Rais wa Zanzibar, Dkt. Mohamed Shein.
 Rais akipokea Rasimu hiyo.....
 Rais Jakaya Kikwete akihutubia baada ya kupokea Rasimu hiyo.
 Eti na huyu jamaa naye alikuwa akisikiliza kwa makini hotuba ya Rais kuhusu Rasimu hiyo...
 Mtangazaji wa ITV na Redio One, Alfred Masako (kushoto) na Dkt. Kitila, wakisikiliza kwa makini hotuba ya Rais.
 Sehemu ya wananchi na viongozi waliohudhuria hafla hiyo.
 Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, Jaji Warioba, akizungumza.
 Umakini wa kusikiliza....
 Rais Jakaya akiteta jambo na Jaji Warioba.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Prof. Ibrahim Lipumba.
                                Picha ya pamoja...... RASIMU YA KATIBA MPYA

No comments:

Post a Comment