Monday 2 December 2013

HAFLA FUPI YA UZINDUZI WA PIKIPIKI KATIKA UWANJA WA UHURU PLATFORM LEO JUMAPILI TAREHE 01.12.2013 BUKOBA.

Mgeni Rasmi Barozi Khamis Kagasheki akiwakilishwa na Mwakilishi wake ambaye ni mjumbe wa NEC Mkoa Kagera Bw. Abdu Kagasheki (kulia) akikata utepe tayari kwa kufungua Hafla hiyo fupi ya uzinduzi wa pikipiki katika uwanja wa Uhuru Platform leo Jumapili asubuhi.
Tayari Utepe umekatwa ..tayari kwa ufunguzi huo.
Mgeni rasmi Bw. Abdu Kagasheki akitoa neno baada ya kukata utepe!!
Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Kagera Bw. Winston Kabantega (kushoto) akiwa naBw. Abdu Kagasheki

Mwakilishi wa Kampuni ya Kishen Herita Hamberile akizungumza na umoja wa wanapikipiki mkoa wa Kagera pamoja na wanachi waliojitokeza kwenye uwanja huo wa Uhuru leo jumapili.

Mzigo wenye huu hapa zimetolewa pikipiki 50
Jumla ya pikipiki 50 zimetolwa leo kwa vijana ikiwa ni lengo la ajira kwa vijana mjini Bukoba kutoka kwa kampuni ya Kishen ya jijini Dar es salaam yenye ofisi zake hapa mjini Bukoba.

Mwendesha pikipiki Gregory Mwombeki ambaye ni Katibu wa chama cha waendesha pikipiki CPMB Kagera akisoma Risala mbele ya Mgeni rasmi.
Baadhi ya madreva waendesha pikipiki wakisikiliza Risala

Katibu wa CCM Wilaya, Bi. Janeth Kayanda nae alikuwepo
Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Kagera Bw. Winston Kabantega kulia akiwa na Ramadhani Kambuga (kushoto).
Wacheza ngoma wakiburudisha
Kikundi cha wanangoma kikiongozwa na Babu Rweyemamu kikitumbuiza

Mwl. Joyce Roboz (kulia) nae alikuwepo kwenye hafla hiyo na hapa alionekana kuburudika vilivyo
Babu Rweyemamu akiimba nyimbo inayopendwa zaidi na wakazi wa Bukoba



Ngoma ya Kihaya ikiendelea kukolea kwenye uwanja wa uhuru platform mjini Bukoba leo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa pikipiki.

No comments:

Post a Comment