Monday 23 September 2013

MAADHIMISHO YA UFUNGUZI WIKI NENDA KWA USALAMA BARABARANI MKOANI KAGERA 2013 YAFANA.


BARAZA la Taifa la Usalama Barabarani limeanzimisha Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani mikoa yote nchini Tanzania leo tarehe 23.09.2013 ambayo yanatarajiwa kufika kikomo wiki ijayo tarehe 27.09.2013. Lengo kuu la maadhimisho haya ni kuendelea kutoa elimu ya matumizi sahihi ya barabara kwamakundi yote ya watumiaji wa Barabara.
Pamoja na kuwa maadhimisho haya yatafanyika mikoa yote nchini kwa kupitia Kamati za mikoa za usalama barabarani zilizopo kila mkoa, ambapo kitaifa maadhimisho haya yanafanyika mkoani Mwanza.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni


“Usalama Barabarani unaanzia kwangu, kwako na sisi sote ”
(Road safety starts with me, you and all of us)
Maandamano kulekea uwanja wa Kaitba Bukoba mjini.
Wanafunzi wa shule ya kolping waliokuwa na shughuli ya kupiga tarumbeta wakati wa sherehe za maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama zilizofanyika kwenye viwanja vya kaitaba leo hii Bukoba.
Kauli mbiu hii inasisitiza kuwa kila mtumiaji barabara ana wajibu wa kuhakikisha Usalama Barabarani unaimarika.






Kuelekea Uwanjani Kaitaba...


Kuelekea Uwanjani Kaitaba ambako maadhimisho hayo yamefanyikia hii leo
Wanafunzi kutoka Shule za Msingi nao walikuwepo kwa swala zima na kupata mafunzo hayo na kupata elemu ya Usalama Baabarani kuzingatia kauli mbiu ikisema.....“Usalama Barabarani unaanzia kwangu, kwako na sisi sote ”

Wanafunzi wa shule ya kolping waliokuwa na shughuli ya kupiga tarumbeta wakati wa sherehe za maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama zilizofanyika kwenye viwanja vya kaitaba leo hii Bukoba.

Wanafunzi wa shule ya kolping waliokuwa na shughuli ya kupiga tarumbeta wakati wa sherehe za maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama zilizofanyika kwenye viwanja vya kaitaba
Wanafunzi wa shule ya kolping waliokuwa na shughuli ya kupiga tarumbeta wakati wa sherehe za maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama zilizofanyika kwenye viwanja vya kaitaba leo hii Bukoba.
Wanafunzi wa shule ya kolping.
Waimbaji wa KAKAU Band kutoka hapa Bukoba wakiimba uwanjani Kaitaba hii leo




Kakau Band wakifanya yao uwanjani Kaitaba.
Mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Massawe akiingia Uwanjani na hapa akisalimiana na baadhi ya viongozi.

Kuelekea uwanja wa Kaitaba.
Dreva Bw. Mbelwa (kushoto) nae alikuwepo uwanjani hapo kuhakikisha swala hili la Usalama barabarani linaadhimishwa kwa kutoa elimu kwa wote!
Vijana wa Baodaboda wakitoa yaliyo moyoni mwao kwenye bango!!

Waimbaji wa Kakau Band wakiendelea kutumbuiza uwanjani hii leo
Kakau Band wakitumbuiza kwa nyimbo zao za kuhamasisha swala zima la Usalama Barabarani.
Wito kwa abiria kutoshabikia vitendo vya ukiukwaji wa sheria kama vile mwendokasi, abiriawanatakiwa kukemea na kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi pindi waonapo ukiukwaji wa sheriana kanuni za usalama barabarani wasisite kutuma taarifa hizi kupitia namba za simu zaviongozi wa Polisi katika mikoa husika ambazo zimebandikwa kwenye baadhi ya mabasi.Waimbaji wa Kikundi cha Kakau wakiimba hapa kwa furaha.

Bw.Winston Kabantega Mkurugenzi wa CHUO cha Mafunzo ya Udereva cha Lake Zone ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Kagera, akizungumza na umati wa watu waliojitokeza uwanjani Kaitaba leo hii mchana. Pia mkuu huyo amewasihi wapanda pikipiki kuacha tabia ya kupakia abiria zaidi ya mmoja (mshikaki), kufuataalama na ishara zinazotolewa na wasimamizi wa sheria, kuzingatia uvaaji wa kofia ngumu(helmet) na pia kuacha tabia ya kujichukulia sheria mikononi pindi wanapohusika katika ajali.
Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Massawe wa kwanza kulia toka Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho haya ya Wiki nenda kwa usalama.
Baadhi ya viongozi wa serikali.
Pia Viongozi wamewashauri madereva wote wa magari kujiepusha kuendesha magari wakiwa wamechoka au wakiwa wametumia kilevi. Tunawahimiza madereva na abiria kufunga mikanda ya usalama wawapo safarini, kwani kwa kiasi kikubwa mikanda hii husaidia kupunguza vifo na ukubwa wa madhara ya majerahakatika matukio ya ajali. Kabantega ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Kagera, alisema chuo chake kinafanya kazi ya kuwahamasisha madereva hao ili wajiunge na vyuo vinavyotoa mafunzo ya udereva kwa kuwa vitawasaidia kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.
Kikosi cha zimamoto

No comments:

Post a Comment