Wednesday 28 September 2016

SERIKALI NA KAMPUNI YA HALOTEL YATOA POLE SHILINGI 1,885,000 KWA KILA FAMILIA 17 ZILIPOTEZA NDUGU KWENYE TETEMEKO KAGERA

 Mkuu wa Mkoa wa Kagera meja Jenerali mstaafu Salumu Kijuu amekabidhi kiasi cha shilingi  milioni 17 kwa niaba ya serikali kwa familia za marehemu waliofariki katika janga la tetemeko la ardhi liliotokea 10-9-2016 katika mkoa wa kagera na kusababisha vifo na majanga makubwa,pia kampuni ya simu za mkononi ya Halotel imetoa kiasi cha shilingi  15,045,000 kwa ajili ya pole kwa familia  zilizopoteza ndugu,kila familia imeweza kupata pole ya shilingi 1,885,000, Watu 17 walipoteza maisha wakati wa tetemeko, serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni moja kwa kila familia na kampuni ya simu za mkononi Halotel imetoa kiasi cha shilingi 885,000 kwa kila familia.(katika picha mkuu wa mkoa Kagera Meja Jenerali Salumu Kijuu akikabidhiwa kiasi cha milioni 15,045,000 na mkurugenzi  Bw Tran  Hieu Nghia wa Halotel akiwa na msaidizi wake  Bw  Naswiru Zuberi.)


 Ndugu wa marehemu waliofika kupokea pole.




 Halotel wakikabidhi  15, 045,000.
 Poleni kwa kupoteza ndugu.
Kushoto  ni mkurugenzi msaidizi Bw Naswiru Zuberi wa halotel Kagera, Bw Tran Hieu Nghia mkurugenzi na Bw  Johanes Julius afisa wa halotel Kagera.

No comments:

Post a Comment