Wednesday 28 September 2016

ALIEKUWA KATIBU TAWALA KAGERA MBALONI NA WENZAKE.

 Aliekuwa katibu tawala  Mkoa wa Kagera Bw   Amantius Msole na wenzake wamekamatwa na polisi kufuatia agizo la rais John Mgufuli kutengua uteuzi wake na wenzake baada ya kugundulika kufungua akaunti tofauti ya Maafa ya tetemeko la ardhi mkoa wa kagera,Bw Msole, alikuwa mkurugenzi wa manispaa ya Bukoba Bw Steven Makonda,mhasibu wa mkoa, na meneja wa benki ya CRDB Bukoba wamekamatwa lwa ajili ya uchunguzi kufanyika kufuatia tuhuma ya kufungua akaunti itwayo Kamati Maafa Kagera kwa lengo la kujipatia fedha.(katika picha ni aliekuwa Katibu tawala wa Mkoa wa Kagera Bw Msole akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi akitolewa ofisini kwake na kurudishwa polisi baada ya upekuzi.)
 Kikazi zaidi.
Tunaendelea kumtafuta kamanda wa mkoa wa Kagera kwa habari zaidi.

No comments:

Post a Comment