Thursday 9 July 2015

JK AZINDUA UKUMBI WA KISASA WA MIKUTANO WA CCM MJINI DODOMA


 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na viongozi mbali mbali wa mkoa wa Dodoma mara baada ya kuwasili kwenye sherehe za uzinduzi wa jengo jipya la mikutano la CCM.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiongoza sherehe fupi za uzinduzi wa jengo jipya la mikutano la CCM mjini Dodoma
 Mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya CRJE Ndugu Hu Bo akihutubia kwenye sherehe za uzinduzi wa Jengo la kisasa la mikutano la CCM mjini Dodoma.
 Viongozi wakifurahia hotuba ya Mkurugenzi wa CRJE
 Balozi wa China Nchi Mhe. LU Youqing akizungumza wakazi wa uzinduzi wa Jengo jipya la Ukumbi wa mikutano la CCM mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati wa sherehe fupi za uzinduzi wa jengo la ukumbi wa kisasa wa mikutano wa CCM mjini Dodoma.
 Bendera za CCM zikipepea nje ya ukumbi wa jengo jipya la kisasa la mikutano Dodoma Convention Center.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa salaam za kumkaribisha Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kuja kutoa hotuba ya ufunguzi wa Ukumbi mpya wa kisasa wa mikutano wa CCM mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais Jakaya Kikwete akihutubia wakati wa sherehe za ufunguzi wa ukumbi wa kisasa wa mikutano wa CCM mjini Dodoma
 Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibonyeza tufe kuashiria kufunguliwa rasmi kwa jengo jipya la ukumbi wa kisasa wa mikutano la CCM mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea ufunguo kutoka kwa Mkurugenzi wa kampunzi ya ujenzi ya CRJE kutoka China Ndugu Hu Bo kama ishara ya kukabidhiwa jengo la ukumbi wa kisasa la mkutano la Dodoma Convention Center.

No comments:

Post a Comment