Sunday 27 July 2014

KASHAI FC WATUPWA NJE KWA MIKWAJU YA PENATI (5-4) NA TIMU YA MIEMBENI FC KAGASHEKI CUP, MIEMBENI WASONGA HATUA YA ROBO FAINALI!

Na Faustine Ruta, Bukoba
TIMU ya Kashai Fc maarufu kama Abanyaruganda imetupwa nje ya Mashindano ya Ligi ya Kagasheki leo kwenye Hatua ya Robo fainali baada ya kutoshana nguvu ya bao 1-1 na timu ya Miembeni. Kipindi cha kwanza kilimalizika ya bila kufungana. Timu ya Kashai ndio ilianza kupata bao katika kipindi cha pili kupitia mchezaji wake Shamte Odilo na wao Miembeni kusawazisha bao kupitia kwa Rashid Mandawa katika kipindi hicho hicho cha pili na mtanange kumalizika kwa dakika 90 kwa sare ya bao 1-1 na hatimaye Mtanange kwenda kwenye Mikwaju ya penati ambayo timu ya Miembeni imeibuka kidedea kwa penati 5-4. Ushindi huu wa Timu ya Miembeni unawakutanisha na Mabingwa watetezi Bilele Fc walioshinda jana bao 1-0 timu ya Kahororo na sasa watakutana katika Nusu Fainali wiki Ijayo kati ya Bilele Fc na Miembeni walioshinda leo.

Patashika kwenye lango la Miembeni Fc

Jackson (kulia) akimwesabu Msengi Gerard wa Kashai katika kipindi cha kwanza

Hapa hukatizi!

Mchezaji wa Miembeni Jackson Kanywa kwenye mbio za kutaka kumtoka mchezaji wa Kashai Fc.

Kipindi cha pili lango la Timu ya Miembeni liliandamwa sana na kupata bao lao

Mtanange ulikuwa wa kasi sana kipindi cha kwanza kila timu ikipania kumfunga mwenzake, Kitu ambacho katika kipindi hicho cha kwanza hakuna aliyeliona lango la Mwenzake.Ilikuwa ni Ngoma na Nyimbo kwa Mashabiki hawa wa Kashai maarufu AbanyarugandaMizuka ya Mashabiki wa Kashai Fc wakiipamba timu yao leo kwenye mchezo wake wa Robo Fainali dhidi ya timu ya Miembeni FcViongozi wakiwa Jukwaa Kuu wakitazama Mtanange kati ya Kashai Fc vs Miembeni Fc, wa pili kutoka kulia ni Bw. Ernest Nyambo.Mashabiki Jukwaa kuu wakitazama Mtanange!Mashabiki wa Kashai wakiishangilia timu yao leo hii ambayo imetupwa nje kwa mikwaju ya penati baada ya kuchezea sare ya 1-1 za dakika 90.Kisa Mwamuzi Mshika kibendera alinyanyua kuashiria kuotea huku wachezaji wa Miembeni wakipingana nae!!kabla ya Timu ya Mimbeni hawajapata bao walikwaruzana na Mwamuzi wa pembeni mshika kibendera..Wachezaji wa Miembeni wakishangilia bao lao la kusawazisha lililotiwa kimiani na Rashid MandawaWachezaji wa Miembeni wakicheza Muziki baada ya kusawazisha bao katika kipindi cha pili kwa kufanya 1-1 ndani ya dakika 90.Ilikuwa ni staili ya aina yake kushangilia Nyomi ya Mashabiki Uwanjani Kaitaba wakitazama Mechi ya leo hii kati ya Kashai Fc na MiembeniMashabiki wa Timu ya Kashai wakitokelezea!! Mashabiki wakitazama Kipute cha leo hiiKatika Michuano hii ya Ligi ya Kagasheki 2014 Kata ya Kashai ndio huwa na Mashabiki wengi

No comments:

Post a Comment