Wednesday 19 June 2013

WAFUASI WA CHADEMA BUKOBA WAPATWA NA BUTWAA UWANJA WA NDEGE BUKOBA,BAADA YA RWAKATARE KUTOONEKANA AKISHUKA KWENYE NDEGE NA KUTAWANYIKA NA BAADA YA MUDA RWAKATARE AKAONEKANA MTAANI AKIELEKEA UWANJA WA UHURU BUKOBA

 Ni majira ya saa sita na nusu mchana katika uwanja wa ndege wa bukoba wafuasi wa chadema walikuwa wakifika katika maeneo hayo wakiwa na mabango,baiskeli ,pikipiki na wengine kwa magari na miguu kuja kumpokea wilfred rwakatare mwenyekiti wa chadema mkoa wa kagera ambae alikuwa gerezani siku 92 ,katika hali ya kushangaza mara baada ya ndege kuwasili uwanja wa ndege bukoba katika ndege hiyo walishuka abiria watatu na miongoni mwao rwakatare hakuwepo,na habari zilienea uwanjani hapo kuwa hakuna ndege yoyote itakayotua tena maana kuanzia saa nane mkandarasi wa uwanja anaendelea na ujenzi wa uwanja,hali hiyo ilisababisha watu kuondoka uwanjani hapo kwa kujiuliza maswali mengi ambayo majibu yake hayakuwa rahisi,mara baada ya muda,wafuasi walitangaziwa na mwenyekiti wa chadema wilaya ya bukoba ndugu sherejei kuwa  ndugu rwakatare amechelewa ndege ila chama kinafanya mpango wa kukodi ndege ili afike bukoba,kauli hii ilileta maswali ,maana tayari ilishakuwa saa nane na nusu na uwanja ulishafungwa kwa shughuli za ujenzi,hapo watu walitawanyika na kuondoka,ghafla katika hali kusitaajabu rwakatare akaonekana mtaani akiwa kwenye gari ya wazi akipunga mkono na kuelekea uwanja wa uhuru  uswahilini ambako mkutano wa hadhara ulikuwa unafanyika huko,kwa mujibu wa mtu wandani kwa mashariti ya kutotajwa jina rwakatare aliwasili bukoba kwa basi toka jana na kufichwa mahala.



                     watu waliamua kuzimua na kutafuta stimu wakiwa uwanja wa ndege wakisubiri

           muda ukazidi kwenda,na watu wakazidi kunywa huku wakiimba rwakatare mjerajera original
 baada ya mambo kukolea watu wakakumbuka waliokufa arusha,wakajifunga vitambaa vyeusi
 ni full vituko uwanja wa ndege wa bukoba leo,ila rwakatare hakutokea ,baadae akaonekana mtaani
                                                       ngoma zikachezwa kumsubiri mgeni
                                                                  full mzuka

 sherejei ikabidi atangaze, jamani ndege imemuacha ila chama kinatafuta namna ya kukodi ndege
                                                            ulinzi ulikuwepo
                                                             matax dreva wa sokoni
                                 ndege ilipowasili walishuka abiria 3 rwakatare hakuwemo
 alikuwa ni abiria wa mwisho katika ndege hiyo ,rwakatare hakuwemo,watu walikata tamaa na kutawanyika
                                                watu wakiwa uwanja wa mashujaa uswahilini


                                                          rwakatare akiwa uwanja wa uhuru plat form bukoba


                                     zainabu almas akitangaza kuama cuf na kwenda chadema


                                         wananchi wakisubiri rwakatare azungumze
                                      vareliani  wa vision redio akipata maelekezo kutoka kwa sherejei
                                              mmoja wa wasemaji akiongea
                                                        akipanga cha kuongea kabla hajasimama




 alisimama rwakatare kikubwa alisema na kutoa ushuhuda kuwa mungu yupo na kila anaeamini na kumuomba atamsaidia,alizungumza mengi aliyokutana nayo katika siku 92 akiwa gerezani,lakini mwisho alisema ametunga kitabu cha maisha akiwa gerezani na anaandika kitabu cha maisha yake hivyo kinatumia gharama kuchapishwa akapitisha mnada kwa kunadi vitu, kama asali,mafuta ya kula, mifagio nk ili pesa itakayopatikana isaidiekuchapisha kitabu chake.chezeea rwakatare weweee

No comments:

Post a Comment