Tuesday 28 March 2017

WANABUKOBA MPYA WAIPONGEZA SHULE YA SEKONDARI KATA HAMUGEMBE ,YAFANYA VIZURI MITIHANI KIDATO CHA NNE MANISPAA YA BUKOBA

 Wana Bukoba mpya wamefurahishwa na matokeo ya kidato cha nne 2016 ya shule ya sekondari ya Hamugembe ambayo imekuwa ya kwanza katika Manispaa ya Bukoba,Mwenyekiti wa  umoja wa Bukoba mpya wakati akiongea na walimu na wanafunzi wa shule ya sekondari Hamugembe Bw Yunus Kabyemela amesema amewakilisha wanaBukoba mpya ambao wanaishi maeneo ,mbalimbali hapa nchini na nje ya nchi wamefurahishwa na matokeo mazuri ya kidato cha nne 2016 ,na kwa kuzingatia changamoto nyingi zilizo kwenye shule za kata nchini lakini pamoja na changamoto hizo bado shule ya Hamugembe wamefanya vizuri, Bw Yunus Kabyemela aliendelea kusema Wana Bukoba mpya kwa kutambua umuhimu wa elimu wameona walimu wanastaili pongezi kubwa na kutiwa moyo kwa kazi kubwa wanayoifanya .Bw Yusus Kabyemela alikabidhi Tuzo kwa mwalimu mkuu wa Hamugembe sekondari Bw Evodius Rwezahura kama ishara ya kutambua na kuwapongeza kwa ushindi walioupata,pia wana Bukoba mpya walitoa bahasha kwa kila mwalimu wa shule hiyo iliyokuwa na chochote kwa kutambua kazi kubwa inayofanywa na walimu, Bw Yunus alisema kwa upande wa shule wanaBukoba mpya wametoa vitabu vya wanafunzi ambavyo watavitumia katika masomo yao, hafra hiyo fupi pia iliudhuliwa na mstahiki meya wa Manispaa ya Bukoba Mh Chief Kalumuna, makamu Meya Jimmy Karugendo ambae pia ni mwana Bukoba mpya, afisa elimu wa sekondari Manispaa ya Bukoba Bw Wandele Rwakatare, Diwani wa kata Hamugembe  Mh Muhaji Kachwamba,walimu na wanafunzi.(katika picha  mwenyekiti wa BUKOBA MPYA  Bw Yunus Kabyemela akikabidhi Tuzo kwa mstahiki meya,Pia kitaifa katika mitihani ya darasa la nne kitaifa, kidato cha pili kitaifa na kidato cha nne kitaifa Manispaa ya Bukoba imekuwa ya kwanza kitaifa 2016.
 Hii ndio Tuzo.
 Wana Bukoba mpya wakiwasili shuleni.
 Kushoto mwenyekiti wa Bukoba mpya Bw Yunus Kabyemela akiteta na mkuu wa shule.
 Makamu meya MH Jimmy Karugendo.
 Wanafunzi wa Hamugembe sekondari.
 Wimbo wa Tanzania nakupenda ukiimbwa.
 Kushoto Mh Diwani kata ya Hamugembe Muhaji Kachwamba ,afisa elimu sekondari Bw Wandele Rwakatare na makamu meya Jimmy Karugendo.
 Mstahiki Meya Mh Chief Kalumuna akitoa pongezi kwa wana Bukoba mpya kwa kutambua na kuthamini eli,mu na kuwashukuru kwa kitendo cha kiungwana walichokifanya.
 Mwenyekiti wa Bukoba mpya akiongea .
 TUZO
 Baadhi ya vitabu vilivyotolewa na wanaBukoba mpya.
 Mkuu wa shule akifurahi Tuzo na wanafunzi.
 Mwl Mkuuakipokea bahasha yake  ya motisha kwa kazi wanayoifanya .
 Walimu wakipokea bahasha yenye kitu kidogo kutoka kwa wanaBuboba mpya.
 Furaha tele, hapana chezea bahasha weweee.
 Mh diwani wa kata akitoa neno la shukrani.
PICHA YA PAMOJA.

No comments:

Post a Comment