Monday 30 March 2015

KATIBU WA CCM MKOA WA KAGERA AKIRI KUWA KAGASHEKI KWA BUKOBA MJINI NI MAFURIKO HAZUILIKI KWA VIGANJA,KATIKA MKUTANO KATA KASHAI.

 Umati mkubwa uliojitokeza kwenye mkutano wa kashai.Katibu wa ccm Mkoa wa Kagera Bw Idd  Ally  Amme amekiri na kukubari katika mkutano wa hadhara  wa chama cha mapinduzi uliofanyika katika uwanja wa Mafumbo kuwa Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini Balozi  Khamis Kagasheki ni kipenzi cha wanaBukoba Mjini, Bw Idd Amme amesema kwa kipindi ambacho ameamia Kagera akitokea Tabora ameshuhudia Mbunge namna anavyokuwa na wananchi wake bila kubagua chama akitekeleza ilani ya chama cha mapinduzi kwa wanaBukoba wote,Huku akishangiriwa na umati mkubwa uliojitokeza kwenye mkutano huu,Mapema Mbunge wa Bukoba Mjini alisimama kusalimiana na wanajimbo alisema Anashangaa na anajiuliza ilikuwaje Kashai ikapoteza mitaa yote kwa umma uliofurika katika mkutano, Mh Kagasheki alikiri udhaifu uliojitokeza katika chama cha mapinduzi katika kata ya Kashai zikiwemo Hujuma mbalimbali  za watu kupiga kura zaidi ya mara tatu, watu kutoka maeneo mengine na kujiandikisha Kashai na wanaccm wengi kutojiandikisha kwa kutojari umuhimu wa uchaguzi huo, Mh Kagasheki akasema  Hakuna atakayerudia kosa tena na hasa katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, amewasihii na kuwaomba wananchi wote kujiandikisha kwa wingi na kuhakikisha chama cha mapinduzi kinashinda uchaguzi kwa nafasi ya rais, ubunge na madiwani.
 Dada alishindwa kuzuia hisia zake  pale Kagasheki alipowasili atika viwanja vya Mafumbo.
 Ilikuwa ni shidaaa
 Umati ukazizima.
 Mwenyekiti wa ccm kata Kashai.
 Charles Mubea wa Tbc akiwajibika.
 Kagasheki oyeeeee, wamama uwaambii kitu kwa Kagasheki.
 Mzee Habibu Mayoro kada wa ccm makini.
 Msanii Kamatilie akifanya mambo yake.
 Ulinzi uliimarishwa.
 Kada wa ccm.
 Katibu wa ccm Bukoba Mjini.
 Kamanda wa UVCCM Bukoba Mjini Phiribert Nyerere akiongea na wananchi.
 Akasimama Mbunge kuongea na wananchi.
 Wakaimba wananchi mafuriko hayazuiwi na viganja.
 Mwenezi wa Mkoa Hamimu Mahamod akaongea na wananchi.
 wafuasi wa vyama vyote walikuwepo.

 Mwenezi wa Mkoa akasema kwa hali ilivyo kwa Bukoba Mjini haoni zaidi ya Kagasheki,maana kazi alizofanya zinajieleza.
 Katibu wa Mkoa akaeleza mafanikio ya ccm tangu uhuru.
Endelea kufuatilia.

No comments:

Post a Comment