Friday, 14 June 2013

AJALI MBAYA YATOKEA BARABARA YA ARUSHA MAENEO YA SOKO KUU BUKOBA



 Gari iliyokuwa inawafuata maharusi kuwapeleka kanisani imejikuta inaishia barabara ya arusha maeneo ya soko kuu bukoba baada ya kugongana na gari jingine,gari ili hatukuweza kupata jina la mmiliki ila inasemekana ni gari la daktari anaefanya kazi shirika la ICAP bukoba



 Huyo mwenye suti nyeusi ndio inasemekana ni dakitari anaemiliki gari nyeusi na huyo mwingine inasemekana ni mfanyakazi wa takukuru bukoba anaemiliki gari nyekundu

















                                                               gari hili liligongwa ubavuni
                                           hapa kila mmoja huongea lake wakati kakuta ajali tayari

                                         dah kabla ya kupaki gari lolote linaweza kutokea.
 kabla wanausalama barabarani mnaelewana watu mnaondoka,naona ilikuwa hivyo si unaona...
                            hapa kama kwenye  harusi hakuna fungu la dharula inakuaga shida
                                                        jamani njooni kuna ajali......



wananchi tena wakishaona kitu ,tena maeneo ya soko, kujikusanya huwa ni dakika chache pamejaa
gari zote zilitoka kwenye eneo la ajali na kuchikichia,yawezekana kwa makubariano maalumu

Thursday, 13 June 2013

BREAKING NEWS: MSANII WA HIP HOP TANZANIA LANGA AFARIKI DUNIA.

Thursday, 13 June 2013


Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba msanii Langa afariki dunia..
Langa Kileo (msanii wa Hip Hop Tanzania, pichani) amefariki dunia leo
Langa alipelekwa hospitali akiwa hajitambui. Anadaiwa kuwa alikumbwa na Malaria kali sana, Hali iliyopelekea kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili jana.
Uchunguzi wa chanzo cha kifo chake bado unaendelea.
Msanii Langa aliwahi kutamba na kikundi cha Wakilisha pamoja na witness na sara ni miongoni mwa wasanii wakongwe wa bongo flava nchini Tanzania.

Mungu amrehemu, Ameen

Thursday, June 13, 2013 HABARI:NELSON MANDELA ALIKIKARIBIA KIFO RIPOTI TOKA KWA MADAKTARI

 

Thursday, June 13, 2013



Ni siku nne zimepita imetokea hali ya sintofahamu baada ya mpiganiaji Uhuru wa South Africa
Babu Nelson Mandela kukimbizwa hospitalini baada ya hali yake kuwa mbaya na kuwekwa
kwenye chumba cha watu mahututi.....
Ripoti kutoka kwenye hospital aliyolazwa Rais huyo wa zamani wa Taifa hilo inasema
usiku wa kuamkia leo siku ya Alhamisi majira ya saa 8 usiku hali ya Mandela ilibadilika
na Team ya madaktari walikusanyika na ilionekana Mapigo ya Moyo kuacha kufanya kazi
kwa muda na Figo kushindwa kufanya kazi kwa dakika zisizopungua 10....
baada ya kupigania
uhai wake hali ilirudi kuwa ya kawaida na kuendelea kupata matibabu chini ya madaktari
Bingwa...
Pia Raisi wa sasa wa South Africa Bwana Jacob Zuma ameongea na kusema ''Naiamini
team ya madaktari inayomuangalia mzee wetu na nina imani Mungu atamuepusha
na mabaya yote na kurudi kwenye hali yake kama kawaida...,nampenda mzee mandela,
wote tunampenda mandela na dunia nzima inampenda kwahiyo kwa pamoja tuungane kumuombea...!!

NI TEKNOLOGIA INAYOTUMIKA KUKAMATA SENENE,LAKINI YENYE KUITAJI GHARAMA



 Unapozungumzia senene kwa muhaya ni kitu kikubwa na cha heshima,miaka ya huko nyuma sana kipindi cha msimu wa senene nazungumzia mwezi wanne na mwezi wa kumi na moja mpaka kumi na mbili kila mwaka senene walikuwa wakipatikana kwenye mbuga zenye nyasi,hivyo watu walikwenda maeneo hayo kipindi cha msimu na kuwatafuta senene,na miaka hiyo watu walitembea mwendo mrefu sana kufuata senene maana si mbuga zote ungeweza kuwapata, kadri siku zilivyozidi kwenda binadamu wanakuwa wabunifu,na miaka ya tisini ikaingia teknologia ya kukamata senene kwa kutumia mtambo maalumu kama wanavyosema wahusika. teknologia hiyo yenye kutumia taa zenye mwanga mkali sana zinafungwa kitaalamu na mapipa ambayo senene wanapofuata mwanga uanguka kwenye mapipa hayo,staili hii inakuwa kwa kasi kubwa wakati wa msimu,lakini ni tekenologia inayohitaji pesa ili uweze kununua vifaa.wapo baadhi wanaofanya biashara hii wananunua mpaka jenereta binafsi kuepuka umeme wa tanesco,kwa kiasi kikubwa watu wamefanikiwa kujenga majumba mazuri,kusomesha watoto,kununua magari nakuendeleza biashara zao.


 ni  jenereta zinazotumika wakati wa msimu wa senene,kuepuka gharama za umeme wa tanesco



 ni mapipa ambayo senene wanapofuata mwanga na kuwa wengi hudondoka kwenye mapipa hayo


 hizo ni taa ambazo zimetolewa kioo cha nje,taa hizi uhuzwa dukani kati ya laki moja mpaka laki moja na nusu kwa taa moja


wengi wameboresha maisha yao kwa ajili ya teknologia hii ya kukamata senene,kwa bukoba eneo las nyamkazi ni maarufu kwa mitambo hii,lakini pia teknologia hii imeshasambaa katika wilaya za mkoa wa kagera na nchi jirani kama uganda, rwanda nk,leo ukizunguza senene  makabila mengi wanakula kuliko hata wahaya,na kipindi cha msibu biashara ya nyama na samaki hudorola kwani watu wengi hutumia senene kama mboga.

KAGASHEKI CUP 2013 KUANZA 29-6-2013 KATIKA UWANJA WA KAITABA



Kagasheki cup 2013 inatarajiwa kulindima 29-06-2013,ligi hiyo inayodhaminiwa kwa asilimia mia moja na mbunge wa jimbo la bukoba mjini na waziri wa maliasili na utalii balozi khamis kagasheki, kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya kagasheki cup,marick tibabimare ambae pia ni mwenyekiti wa chama cha mpira bukoba mjini amesema timu zitakazoshiriki ni za kata zote 14 za jimbo la bukoba mjini na amewataka viongozi wa timu  kata zote 14 siku ya jumamosi wakutane katika uwanja wa kaitaba ili waweze kupewa taratibu za maandalizi ya kagasheki cup 2013,katika ligi ambayo uleta hamasa kwa wanajimbo la bukoba mjini ni kagasheki cup,na hii inatokana na maandalizi ambayo ufanyika na zawadi nono ambazo hutolewa na mh kagasheki, kwa ligi iliyokwisha mh kagasheki alitoa zawadi ya mshindi wa kwanza alijinyakulia kitita cha shilingi milioni tano,wa pili milioni tatu ,na watatu milioni mbili na nusu,lakini pia mh kagasheki hutoa jezi,viatu na mipira kwa timu zote .lakini pia mh kagasheki ugharamilkia gharama zote za uendeshaji wa timu ,kama posho za waamuzi,maji kwa ajili ya timu zote na gharama za uendeshaji uwanja na ndio maana wananchi wote uingia bure kuangalia mechi.timu zinazotarajiwa kushiriki ni bakoba mabingwa watetezi,kashai,miembeni,kitendaguro,ijuganyondo,bilele, zingine ni nyanga,kibeta,kahororo,hamugembe, rwamishenye,kagondo,nshamya na buhembe. kwa upande wa zawadi kagasheki cup mwaka huu zitatangazwa muda mfupi kuanzia sasa.

Wednesday, 12 June 2013

WAANDAAJI WA REDD'S MISS KAGERA 2013 (LWERU ENTERTAINMENT) WATINGA KASIBANTE RADIO 88.5FM BUKOBA LEO

kulia ni omary bakari,kapten mwasa aliekaa,faustin ruta na abdulazack wakiwa ofisi za kasibante redio leo kuwaabarisha wananchi kuhusu redd's miss kagera 2013 inayofanyika 15-06-2013 lina's
Bw. Jamali Kalumuna akizungumza na kuweka wazi kuhusu shindano hilo linalotarajiwa kufanyika tarehe 15.6.2013 kwenye ukumbi wa Lina's uliopo mjini Bukoba.Bw. Jamali Kalumuna(kushoto) akizungumza kuhusu ujio huo wa Redd's Miss Kagera itakayofanyika Jumamosi Tarehe 15.06.2013 leo kwenye ofisi za redio Kasibante fm(88.5) mjini Bukoba
Watangazaji wa Radio Kasibante Fm 88.5 wakiwa kazini leo hii
kushoto ni omary bakari na kapten mwasa wakijibu maswali ya wasikilizaji wa kasibante redio kuhusiana na redd's miss kagera 2013 siku ya jumamosi 15-06-2013
Capt. Mwassa Winton


Capt. Mwassa Winton  akizungumzia Shindano hilo la Redd's Miss Kagera

Kulia ni Bw. Faustine Ruta mwendeshaji wa mtandao wa Bukobasports.com naye akiwakilisha kama mdhamini wa Redd's miss Kagera akiwa naye kwenye radio ya kasibante fm Bukoba leo hii Asubuhi.
Patakuwa hapatashi siku hiyo!!!

Tuesday, 11 June 2013

ASKOFU MKUU WA AUTHODOX JIMBO KUU TAKATIFU LA MWANZA JERONYMOS MUZEEYI AWAASA WANAFUNZI WA KITUO CHA MUJUNGU ACADEMIC CENTRE KUSOMA KWA BIDII



 Askofu mkuu Jeronymos Muzeeyi jimbo kuu takatifu la mwanza amewaasa wanafunzi  wa kituo cha mujungu academic centre kilichoko kata ya kagondo kusoma kwa bidii,ili elimu watakayoipata hapo iweze kuwasaidia katika maisha yao,wanafunzi zaidi ya tisini kutoka katika shule mbalimbali za sekondari ambazo zimefunga wapo hapo shuleni wakiendelea na masoma katika kipindi chote cha likizo,kituo hiki kinafundisha masoma ya sayansi,arts na kilimo


           wanafunzi wa kituo cha mujungu academic centre wakimsikiliza  askofu mkuu



baadhi ya madarasa ya kituo



                                                   askofu akiendesha ibada rasmi ya kuzindua kituo






                                                                 wanafunzi wakiimba wimbo


                                   askofu mkuu alitoa zawadi ya vitabu ili wanafunzi wajifunze




askofu pia alitoa zawadi ya madaftari na kalamu kwa wanafunzi wote,na kulia ni mkuu wa kituo johnstone richard mujungu






                                             kituo hiki wapo wanafunzi wa bweni na wanafunzi wa kutwa
                                     wanafunzi wakipokea zawadi ya dafrari na kalamu kutoka kwa askofu






                                                               someni vitabu...



                                            baba askofu tunaomba utuzindulie

                             baba askofu akizindua rasmi majengo ya kituo cha mujungu academic centre











 mmiliki wa libeneke la jamcobukoba.blogspot.com akiwa katika picha ya pomoja na askofu na mkuu wa kituo akifurahi sana








                                             ni tank kubwa la maji linalojengwa kituoni hapo