Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majdi Mwanga (wa pili kushoto) akipokea sehemu ya msaada wa vitabu vya kiada kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Joel Laurent vilivyotolewa na Kampuni ya Oxford University Press kwa ajili ya Shule za Msingi 48 za mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Hafla hiyo ilifanyika wilayani Bagamoyo juzi. Wa pili kulia ni Meneja Mkuu wa Oxford, Fatma Shangazi na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Bagamoyo, Respicius Selestin. (Picha na Francis Dande)
Meneja Habari, Elimu na Mawasiliano toka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Sylvia Lupembe (kushoto) akiwa pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Majengo ya Bagamoyo wakiandaa vitabu vilivyotolewa kwa shule za msingi 48 katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Joel Laurent akizungumza katika hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majdi Mwanga akizungumza katika hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majdi Mwanga (wa pili kushoto) akimkabidhi kitabu cha kiada mwanafunzi wa Shule ya Msingi Majengo, Moza Mketo baada ya kupokea msaada wa vitabu vilivyotolewa na Kampuni ya Oxford University Press kwa ajili ya Shule za Msingi 48 za mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Hafla hiyo ilifanyika wilayani Bagamoyo juzi. Kulia ni Meneja Mkuu wa Oxford, Fatma Shangazi na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Bagamoyo, Respicius Selestin.