Thursday, 6 October 2016

MWILI WA MAREHEMU GOZIBERT IJUMBA WAWASILI BUKOBA,KUZIKWA JUMAMOSI 8-10-2016

 Mwili wa marehemu Gozibert Ijumba umewasili nyumbani kwake nyamkazi Bukoba majira ya alfajiri  ya leo saa kumi ukitokea Dar  ambako mauti yalimkuta 3-10-2016 katika hospitali ya rufaa Muhimbili,marehemu atazikwa 8-10-2016 kijijini kwao Kanyigo,kabla ya kupelekwa kijijini kwao  siku ya leo itakuwepo ibada takatifu nyumbani kwake Bukoba mjini kuanzia saa sita mchana na watu watatoa hheshima zao za mwisho, na mwili utapelekwa leo kijijini kwao.
 Mjane wa marehemu.

Monday, 3 October 2016

NMB BUKOBA WAANZA MAADHIMISHO YA WIKI YA HUDUMA KWA MTEJA LEO 3-10-2016

Benki ya NMB tawi la Bukoba limeungana na benki zingine nchini kuadhimisha  wiki ya huduma kwa mteja ambayo  hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza ya mwezi wa kumi,Meneja wa tawi la Bukoba Bw Victorine Kimario mapema leo majira ya saa  moja asubuhi wakati wa chai iliyoandaliwa na uongozi wa benki wakiwa na baadhi ya wateja waliokaribishwa chai kwa nia ya ufunguzi rasmi ya wiki ya huduma kwa mteja, Meneja ametumia nafasi hiyo kuwaeleza wateja huduma mbalimbali zinazotolewa na NMB na kuwaomba kuendelea kuiamini  na kuitumia benki yao,Pia amesema mbali na huduma za kibenki zinazotolewa , NMB imekuwa ikishiriki shughuli mbalimbali za kijamii kwa upande wa afya,elimu nk,siku ya Jumamosi wanategemea kutembelea hospital ya mkoa wa Kagera kwa kutoa msaada ikiwa ni maadhimisho ya wiki  ya huduma kwa mteja.(katika picha Meneja mwenye kikombe  akizungumza na wateja wakati wa chai ya asubuhi)


 Ofisi ya benki Bukoba.
 Muonekano wa ndani.
 Meneja akizungumza na wafanyakazi wa benki.



 Bw Juma akimkaribisha mteja.
 Hii ndio kawaida yao , siku zote.
Tabasamu lao ni  uthibisho wa huduma bora NMB.
 Tembelea NMB Bukoba utakutana na hii timu.
 Karibuni wageni.
 Wateja wakimsikiliza meneja wa benki akieleza dhima ya wiki ya huduma kwa mteja.
 Baada ya maelezo, hiki kikafuata.
 Bw G smart akiwa na Bi Penina
 Bw Pk akifurahia kitu.
 Maswali na majibu.