Meneja
Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa habari
(hawapo pichani) kwenye hafla fupi ya makabidhiano ya vyakula
vya kufuturisha watoto yatima katika vitu vilivyopo mikoa ya Dar es
salaam, Mbeya, Arusha, Mwanza katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani
iliyofanyika katika ofisi za Airtel jijini Dar Es Salam ,akifuatiwa na
meneja wa huduma za Jamii wa Airtel bi Hawa Bayumi.
Meneja
Uhusiano wa Jamii wa Airtel bi Hawa Bayumi akimkabidhi mwakilishi wa
Bakwata Ustadh Hassan Malangali vyakula vya kufuturisha katika mwezi huu
mtukufu wa Ramadhani vilivyotolewa kwa vituo vitatu
vya watoto yatima Dar es Salaam (hawapo pichani) vituo vitakavyofaidika
zaidi ni vya Dar es salaam, Mbeya, Mwanza, Arusha hafla ya makabidhiano
iliyofanyika katika ofisi za Airtel Morocco jijini Dar Es Salam .
Meneja
Uhusiano wa Jamii wa Airtel bi Hawa Bayumi akiwakabidhi
Saida Makope mmoja wa wakilishi wa kituo cha watoto yatima mjini Dar Es
Salaam katika hafla fupi ya makabidhiano ya vyakula vya kufuturisha
katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani vilivyotolewa kwa vituo vitatu
vya watoto yatima jijini Dar Es Salaam iliyofanyika
katika ofisi za Airtel Morocco jijini Dar Es Salam akifuatiwa na
mwakilishi wa Bakwata ustadhi Ustadh Hassan Malangali .
Wateja
Airtel sasa kupata muda wa dua, nukuu za qurani, mawaidha kwa kutuma
neno Ramadhani kwenda 15322 kwa shilingi 153 tu kwa siku.
Kampuni za simu za mkononi za Airtel Tanzania kupitia Kitengo chake cha
huduma kwa Jamii wametoa msaada kwa vituo vitatu jijini Dar Es Salaam
vya watoto yatima katika mwezi mtukufu wa Ramadhani vikifuatiwa na vituo
vingine katika mikoa ya Arusha, Mwanza na Mbeya ili kusaidia watoto
wanaolelewa kwenye vituo hivyo.
Msaada
huo umetolewa kwa lengo la kuwalenga watoto kutoka mikoa minne ambayo
ni Dar Es Salaam, Arusha, Mwanza na Mbeya kwa watoto hawa wanaohitaji
upendo hususani katika kipindi hiki cha mfungo wa
Ramadhani. Baadhi ya vitu vilivyotolewa ni Mchele,Sukari,
maharagwe,unga, mafuta ya kupikia,maziwa, juice, majani ya chai na
sabuni vyenye dhamani ya shilingi milioni tano na nusu.
Akizungumza
katika hafla hiyo ya makabidhiano iliyoandaliwa katika
makao makuu ya Airtel jijini Dar Es Salaam, Meneja uhusiano wa huduma
kwa Jamii bi Hawa Bayumi alisema "kwa kutambua umuhimu wa Jamii
tunayofanya nayo biashara kampuni ya Airtel tumeamua turudishe kiasi cha
faida tunayopata kwa wananchi ili iwasaidie.
Akifafanua alisema kwa muda wa miaka 11 iliyopita tumeweza kusaidia
Jamii mbalimbali ya watanzania ndani ya mfungo wa Ramadhani na bila
kuacha nyanja za elimu, michezo kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira
magumu na kukosa huduma mbalimbali za kijamii.
Kwa mwaka huu kupitia Kitengo chake cha huduma kwa Jamii tutarudisha
tulichokipata na tutaweza kufikia watoto zaidi ya 300 wa mikoa ya Dar Es
Salaam, Arusha , Mwanza na Mbeya na mpaka sasa kwa mwaka huu Airtel
imegharamia zaidi ya shilingi millini 150 katika kukuza kiwango
cha elimu kwa watoto wetu hapa Tanzania," alisema Bayumi.
Bayumi
aliongeza kwa kusema kwamba Airtel inapenda kuwatakia kheri na Baraka
katika mwezi huu mtukufu na tangu kuanza kwa Mwezi mtukufu wa Ramadhan,
wateja wa Airtel wanaweza kufurahia huduma maalumu ya
Ramadhani kwa kutuma neno RAMADHANI kwenda namba 15322 kwa shilingi 153
tu kwa siku. Katika huduma hii mteja atapokea dua, nukuu za qurani,
mawaidha na taraweh salat moja kwa moja kwenye simu yake, kila siku.
Naye katibu mkuu wa Bakwata Sheikh Suleiman Lolila ambaye alikuwa mgeni
rasmi alisema mbali ya hafla hiyo makabidhiano ya chakula imetoa fursa
kwa waislam kutoka maeneo mbalimbali kukutana pamoja na kukumbushana juu
ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Aidha Lolila licha ya kuishukuru Airtel Tanzania kwa misaada inayotoa
kwa Jamii alisema jambo hilo linahitaji pongezi na kutaka liungwe mkono
na kuigwa na kampuni zingine hapa nchini.