Wednesday, 30 April 2014

CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA MKOA WA KAGERA KCU(1990 LTD) CHAFANYA MKUTANO MKUU WA MIZANIA 2012 /2013/

Meneja mkuu wa KCU Vedasto Ngaiza akiwakaribisha wajumbe wa mkutano mkuu wa mizania na kumkaribisha mwenyekiti wa bodi kufungua mkutano.
Mwenyekiti wa bodi ya KCU (1990 LTD) Bw John Binunshu akifungua mkutano
Makamu mwenyekiti wa bodi ya KCU Bw Ngalinda akisalimiana na wajumbe
Mjumbe wa bodi mama Muhazi akisalimia wajumbe wa mkutano
Bw Frank mjumbe wa mkutano mkuu kutokea chama cha msingi Maruku
Mjumbe akichangia baadhi ya maswala muhimu
Mjumbe kutokea Ibwera Bw Sadru Nyangasa akichangia maswala ya kuimarisha ushirika
Mkaguzi wa mahesabu kutoka Coasco akisoma mahesabu ya mizania yaliyokaguliwa na Coasco
Wanahabari wakifuatilia kwa umakini
Muonekano wa mkao katika ukumbi wa Bukoba Coop zamani uliitwa ukumbi wa Yasira Hotel
Watendaji wa KCU
Bw Kanjagaire wa kwanza kulia  meneja kitengo cha kuuza kahawa nje kilichoko Moshi
Wajumbe wakipata chakula baada ya mkutano mkuu wa Mizani

KWA WALE WENYE MWALIKO WA BIRTHDAY PARTY YA KARNE YA MALKIA WA BW SIMBA MAWENYA

Bw Abdulrahim Simba Mawenya  anapenda kuwakaribisha wageni wote mliopata mwaliko wa sherehe ya kuzaliwa ya malkia wake Raazizi mpenzi mke wake Bi Rukia Mawenya tarehe 2-5-2014 katika ukumbi wa Lina's ndani ya paa jipya kuanzia saa 1.00 jioni.KAULI MBIU NI  KUPENDEZA, KULA, KUNYWA NA KUCHEZA. Karibuni sana.

Tuesday, 29 April 2014

IBADA YA MISA YA KUMALIZA MATANGA YA MAREHEMU DATUS BUBERWA NYAMWIHURA

 Baba Paroko akinukuu mistari kwenye biblia
 Baba Askofu msaidizi wa jimbo la Bukoba Methodius Kilain ni miongoni mwa wageni walioshiriki ibada
 Kwaya
 Wageni mbalimbali walioudhuria ibaya ya kumaliza matanga
 ENEO LA KABURI LA MAREHEMU DATUS
 Busara na hekima zimejaa kwa baba Askofu Kilaini
Dada  wa marehemu

 Jamcoblogspot,com inaiombea familia kuwa na subira katika hiki kipindi kigumu cha kumpoteza mpendwa wenu.Datus Buberwa Nyamwihura.

MAMA SALMA AZINDUA CHANJO YA KUZUIA MAAMBUKIZO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI KWA WASICHANA WENYE UMRI WA MIAKA 9-16


 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Ndugu Leonidas Gama akimpokea Mke wa Rais Mama Salma Kikwete kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tarehe 28.4.2014. Mama Salma alikwenda Moshi kuzindua rasmi chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana wa umri wa miaka 9 hadi 16.
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mwakilishi wa Shirika la kuhudumia watoto, UNICEF, hapa nchini Dkt. Sudha Sharma, mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Mandela uliopo katika eneo la Pasua katika Manispaa ya Moshi kwa kulikofanyika uzinduzi rasmi ya chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana.
Maandamano ya vikundi mbalimbali kutoka katika Mkoa wa Kilimanjaro wakipita mbale ya mgeni rasmi Mama Salma Kikwete wakati wa sherehe ya uzinduzi wa chanjo kwenye uwanja wa Mandela huko Pasua mjini Moshi tarehe 28.4.2014.

Maandamano ya vikundi mbalimbali kutoka katika Mkoa wa Kilimanjaro wakipita mbale ya mgeni rasmi Mama Salma Kikwete wakati wa sherehe ya uzinduzi wa chanjo kwenye uwanja wa Mandela huko Pasua mjini Moshi tarehe 28.4.2014.
  Mamia ya watu waliohudhuria sharehe za uzinduzi wa chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi, Mama Salma Kikwete katika sherehe hiyo.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi na wanafunzi waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa chanjo ya kuzuia saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 9 hadi 16 huko Pasua, Moshi tarehe 28.4.2014.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana kwenye sherehe iliyofanyika huko Pasua, Moshi Mjini tarehe 28.4.2014. Wengine katika picha (kushoto kwenda kulia) ni Ndugu Leonidas Gama, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dkt. Rufaro Chatora, Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani hapa nchini, Dkt Kebwe Stephen Kebwe, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Neema Rusibamayila, Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Mama Salma na wa Kwanza kulia ni Mwakilishin wa Shirika la Kuhudumia watoto (UNICEF) hapa nchini  Dkt. Sudha Sharma.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza naza mtoto Salma Abillah mara baada ya kupata chanjo ya kuzuia saratani ya shingo ya kizazi na baadaye kumkabidhi kadi yake ambayo anatakiwa kurudi tarehe 28.10.2014 kwa ajili ya kupata chanjo ya pili.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete anaonekana akitoa chanjo ya matone kuzuia ugonjwa wa polio kwa mtoto Ahmad, miezi 10, aliyefika kwenye sherehe ya uzinduzi wa chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana huko Pasua, Moshi